Saa 1 iliyopitaYunus arejea Bangladesh kuongoza serikali ya mpito

 

Yunus arejea Bangladesh kuongoza serikali ya mpito

Muhammad Yunus aliwasili Bangladesh siku chache baada ya Sheikh Hasina kukimbia nchi

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Muhammad Yunus aliwasili Bangladesh siku chache baada ya Sheikh Hasina kukimbia nchi

Mshindi wa tuzo ya Nobel Muhammad Yunus amewasili nchini Bangladesh kabla ya kuapishwa kuwa kiongozi wa muda wa nchi hiyo.

Yunus mwenye umri wa miaka 84 anawasili siku chache baada ya Sheikh Hasina - mwanamke ambaye alitawala Bangladesh kwa mkono wa chuma kwa miaka 15 - kutorokea India.

Alijiuzulu baada ya wiki kadhaa za maandamano yaliyoongozwa na wanafunzi - ambayo yalisababisha vifo vya mamia - yaliongezeka na kumalizika kwa wito wa kumtaka ajiuzulu

Lilikuwa ni moja ya matakwa ya wanafunzi kwamba Prof Yunus aongoze serikali ya mpito, wakitumai kwamba atarudisha demokrasia nchini Bangladesh baada ya miaka mingi ya utawala wa kiimla.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024