Uingereza: Zaidi ya 90 wakamatwa kufuatia maandamano ya mrengo mkali wa kulia

 

Uingereza: Zaidi ya 90 wakamatwa kufuatia maandamano ya mrengo mkali wa kulia

XX

Chanzo cha picha, PA Media

Zaidi ya watu 90 wamekamatwa baada ya maandamano ya siasa kali za mrengo wa kulia kusababisha ghasia katika miji kadhaa nchini Uingereza siku ya Jumamosi.

Vurugu zilishuhudiwa katika miji ya Hull, Liverpool, Bristol, Manchester, Stoke-on-Trent, Blackpool na Belfast, huku mabomu ya machozi yakirushwa, maduka kuporwa na polisi kushambuliwa katika baadhi ya maeneo.

Waziri Mkuu Sir Keir Starmer ameahidi kuvipa vikosi vya polisi "msaada kamili" wa serikali kuchukua hatua dhidi ya "wenye msimamo mkali" wanaojaribu "kupanda mbegu ya chuki".

Mvutano umekuwa mkubwa baada ya mauaji ya wasichana watatu wadogo kwenye tamasha ya densi yenye mada ya Taylor Swift huko Southport, Merseyside, Jumatatu.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024