Urusi lazima ilazimishwe kuleta amani - Zelensky
Urusi lazima ilazimishwe kuleta amani - Zelensky

Chanzo cha picha, EPA
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky jana usiku alisema "Urusi ilileta vita kwa wengine, sasa vinawarudia,".
Katika hotuba yake ya jioni, Zelensky aliongeza "ni haki tu kuwaangamiza magaidi wa Urusi mahali walipo, pale wanapotekeleza mashambulizi yao".
"Tunaona jinsi hii inaweza kuwa na manufaa kwa kuleta amani karibu. Urusi lazima ilazimishwe kuleta amani ikiwa Putin anataka kuendelea na vita," aliongeza.
Zelensky alisema alikuwa amepewa taarifa na Kamanda Mkuu Oleksandr Syrskyy juu ya "operesheni katika Mkoa wa Kursk", na kwamba kilomita za mraba 1,000 za eneo la Urusi sasa ziko chini ya udhibiti wa Ukraine.
Matamshi ya Syrskyy na Zelensky ilikuwa mara ya kwanza kwa afisa yeyote mkuu wa Ukraine kutaja wazi uvamizi wa Kursk kwa jina.