Uvamizi wa Ukraine Urusi: Tunachojua kufikia sasa
Uvamizi wa Ukraine Urusi: Tunachojua kufikia sasa

Chanzo cha picha, Reuters
- Tishio la Putin: Rais wa Urusi anasema Ukraine itapata "jibu linalostahili" kwa uvamizi wake katika eneo la Urusi - na kwamba vikosi vya Urusi "vitamfukuza adui", katika mkutano na magavana wa kanda.
- Udhibiti wa Ukraine: Gavana wa eneo la Kursk - ambalo Ukraine iliingia Jumanne iliyopita - alimwambia Putin kwamba wanajeshi wa Ukraine sasa wanadhibiti vijiji 28. Wanajeshi wa Ukraine wako umbali wa maili 7.4 (kilomita 12) ndani ya eneo hilo, amesema
- Uhamisho wa watu: Gavana wa Kursk aliongeza kuwa watu 121,000 sasa wamehamishwa kutoka katika nyumba zao - na wengine 59,000 wamesalia. Huko Belgorod, eneo karibu na Kursk, karibu watu 11,000 waliambiwa kuondoka asubuhi ya Leo.
- Nini kinafuata? Tunasubiri kusikia maelezo yoyote kutoka Ukraine leo kuhusu uvamizi wao. Mwanahabari wetu Sarah Rainsford anaangalia kama hii itabadilisha maoni ya umma wa Urusi kuhusu vita - anasema ni wazi baadhi wanajiuliza maswali.