Viongozi wa upinzani Tanzania waachiliwa kwa dhamana,
Viongozi wa upinzani Tanzania waachiliwa kwa dhamana,

Chanzo cha picha, AFP
Viongozi wakuu wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema nchini Tanzania akiwemo mwenyekiti wake Freeman Mbowe na makamu wake Tundu Lissu wameachiwa kwa dhamana baada ya kuzuiliwa kabla ya kufanyika kwa mkutano wa vijana.
Takriban watu 520 walikamatwa katika msako mkali uliofanyika nchi nzima ili kuzuia Chadema kufanya maandamano katika mji wa kusini-magharibi mwa Mbeya siku ya Jumatatu.
Polisi wamesema baadhi yao walisalia rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Kukamatwa kwa watu hao kuliibua hofu kuwa Tanzania inarejea katika utawala dhalimu wa hayati Rais John Magufuli, licha ya mrithi wake Samia Hassan kuondoa zuio la mikutano ya upinzani na kuahidi kurejesha siasa za ushindani.
Polisi walipiga marufuku mkutano wa Chadema wakisema ulikuwa na nia ya kusababisha vurugu.
Walitoa mfano wa mwito wa watu kukusanyika pamoja kama ilivyofanyikana "vijana nchini Kenya" - wakimaanisha wiki za maandamano mabaya dhidi ya serikali kama ilivyofanyika katika nchi jirani ya Afrika Mashariki.
Umoja wa vijana wa Chadema umesema ulitarajia watu 10,000 kuhudhuria mkutano huo, chini ya kauli mbiu ya "chukua jukumu la maisha yako ya baadaye".
Siku ya Jumanne, chama kilichapisha kwenye X kwamba ofisi zake Mbeya "zimezingirwa na polisi na hawaruhusu watu kuingia".
Msemaji wa Chadema John Mrema alithibitisha kuachiliwa kwa viongozi kadhaa wa chama - ikiwa ni pamoja na Bw Mbowe na Bw Lissu - lakini akasema kwamba wengine kadhaa walisalia kizuizini.
Hata hivyo, polisi walisema “viongozi wote wakuu wa Chadema waliokamatwa baada ya kuhojiwa na taratibu nyingine wamerudishwa walikotoka”.
Chidema alisema Lissu alikamatwa Jumapili, na Mbowe Jumatatu alipofika uwanja wa ndege wa Mbeya kwa ajili ya kumuokoa mwenyekiti wa chama na viongozi wengine wawili akiwemo kiongozi wa tawi la vijana wa chama hicho John Pambalu.
Lissu, ambaye alinusurika katika jaribio la kuuawa mwaka 2017 baada ya kupigwa risasi 16, alirejea Tanzania mwaka 2023 baada ya kukaa uhamishoni kwa miaka miwili nchini Ubelgiji.
Rais Samia, aliyeingia madarakani kufuatia kifo cha ghafla cha Bw Magufuli mnamo 2021, alisifiwa kwa kuachana na sera nyingi za mtangulizi wake.
Lakini kutokana na kukamatwa kwake, baadhi ya wanasiasa wa upinzani wamemkosoa, wakitilia shaka dhamira yake ya kuleta maridhiano ya kisiasa.Tanzania inatarajiwa kufanya kura za urais na wabunge mwishoni mwa mwaka ujao