Kiongozi wa Hamas Yahya Al-Sinwar auawa na vifaru baada ya kufanya makosa, IDF yaiambia BBC

 

Kiongozi wa Hamas Yahya Al-Sinwar auawa na vifaru baada ya kufanya makosa, IDF yaiambia BBC

g

Chanzo cha picha, Reuters

Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) ametoa maelezo zaidi kuhusu jinsi Sinwar alivyouawa, katika mazungumzo na kipindi cha BBC cha Newshour.

Maj Doron Spielman anasema IDF imekuwa ikifanya kazi katika Rafah kwa lengo la kuwakamata "magaidi wakuu zaidi" - akiwemo Yahya Sinwar.

Spielman anasema katika operesheni zao, vikosi vya IDF vilifunga barabara, vililipua mahandaki na kudhibiti harakati zake katika "eneo dogo zaidi na dogo zaidi ", na kumlazimisha Sinwar "kutembea kama mkimbizi" na hatimaye "kufanya kosa".

"Kusema kweli, ni jana tu alifanya hivyo. Aliondoka kwenye handaki, akaenda kwenye jengo la ghorofa, na [Hamas] akawafyatulia risasi wanajeshi wa Israeli. Kifaru kilijibu mashambulizi, na akauawa katika shambulio hilo."

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024