Marekani yashambulia hifadhi za silaha za Wahouthi zilizofichwa chini ya ardhi

 

Marekani yashambulia hifadhi za silaha za Wahouthi zilizofichwa chini ya ardhi

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Ndege za Marekani

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin, amethibitisha kuwa vikosi vya jeshi la taifa hilo zikiwemo ndege aina ya B-2 vimeshambulia hifadhi za silaha za chini ya ardhi za wapiganaji wa Kihouthi nchini Yemen.

Bw Austin amesema operesheni hiyo ilihusisha ulipuaji wa "usahihi" wa hifadhi tano "zilizoimarishwa" chini ya ardhi, zenye lengo la kupunguza uwezo wa kundi hilo kushambulia meli katika eneo hilo.

Amesema hifadhi hizo zina aina mbalimbali za silaha ambazo Wahouthi hutumia kulenga meli za raia na za kijeshi katika eneo lote.

"Hii ilikuwa hatua ya kipekee kuhusu uwezo wa Marekani kulenga vifaa ambavyo wapinzani wetu wanajaribu kuficha, bila kujali kina chake cha chini ya ardhi ," aliandika katika taarifa yake.

Popular posts from this blog

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024