Ugonjwa wa ajabu wa ‘kucheza densi’ unasumbua mamia nchini Uganda

 

Dec 17, 2024 05:08 UTC
  • Ugonjwa wa ajabu wa ‘kucheza densi’ unasumbua mamia nchini Uganda

Takriban watu 300 wameambukizwa ugonjwa wa ajabu wa ‘kucheza ngoma’ nchini Uganda huku serikali ikianzisha uchunguzi kubainisha chanzo chake.

Wenyeji wanauita ugonjwa huo ‘Dinga Dinga,’ yaani ‘kucheza densi. Jina hilo linatokana na ukweli kwamba dalili zake ni pamoja na homa na kutetemeka hali ambayo husababisha kuwepo ugumu wa kutembea, ilisema.

Kwa sababu zisizojulikana, walioathiriwa na ugonjwa huo ni wanawake na wasichana. Wakuu wa afya nchini humo waliutambua ugonjwa huo kwa amra ya kwanza mwaka jana.

Mlipuko huo wa sasa ulioanza miezi kadhaa iliyopita, uko katika Wilaya ya Bundibugyo kusini magharibi, ambayo inapakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Hakuna kesi zilizoripotiwa katika maeneo mengine ya nchi hiyo.

Afisa Afya wa Wilaya, Daktari Kiyita Christopher ameliambia gazeti la Daily Monitor kuwa hadi sasa hakuna vifo vilivyotokea kutoka na Dinga Dinga.

Alisema mara nyingi ugonjwa huo ni wa kujiponya, na kuongeza kuwa kwa wale waliokuwa katika hali mbaya, madaktari walifanikiwa kuwaponya kwa kutumia  dawa za antibiotiki.

Hata hivyo, daktari huyo amewaonya wenyeji dhidi ya kugeukia dawa za kienyeji ili kuponya ugonjwa huo.

Sampuli kutoka kwa walioambukizwa zimechukuliwa ili kutumwa kwa maabara zinazoendeshwa na Wizara ya Afya ya Uganda kwa uchunguzi zaidi wa ugonjwa huo.

Popular posts from this blog

Vita vya Urusi na Ukraine: Matukio matano muhimu ya faida na hasara kwa Putin 2024

Jeshi la Wanamaji la Marekani limesema linakabiliwa na vita 'kali zaidi' tangu Vita vya Pili vya Dunia dhidi ya Wayemeni

Wanawake 100 wa BBC 2024: Ni nani yuko kwenye orodha mwaka huu?