Posts

Rais wa Venezuela: Marekani na EU zinanyamazia kimya jinai za Kinazi za Israel huko Gaza

Image
 ay 30, 2024 02:30 UTC Rais wa Venezuela amezilaani Marekani na Umoja wa Ulaya kwa kutofanya lolote kukomesha mauaji "ya kutisha" ya Israel dhidi ya Wapalestina. Nicolas Maduro amelaani vikali mauaji yanayotekelzwa na Israel katika Ukanda wa Gaza na kuyafananisha na jinai za kutisha zaidi katika historia. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Maduro alielezea hatua ya jeshi la Israel kulenga kambi ya watu waliokimbia makazi yao katika mji wa Rafah katika Ukanda wa Gaza mauaji ya umati na kuongeza kuwa hivi sasa katika eneo zima la Ukanda wa Gaza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari ya kutisha zaidi ambayo ubinadamu umeshuhudia tangu wakati wa Hitler." " Amebainisha masikitiko yake kuwa Israel inaendeleza mauaji ya kimbari tika Ukanda wa Gaza mbele ya macho ya ulimwengu bila mtu yeyote kuizuia." Aliikosoa Marekani na Umoja wa Ulaya na kusema pamoja na ku

Ubalozi wa Israel nchini Mexico wateketezwa moto katika maandamano ya kupinga mauaji ya Rafah

Image
Waandamanaji waliokuwa na hasira wameuchoma ubalozi wa utawala haramu Israel katika jiji la Mexico City nchini Mexico wakati wakibanisha malamiko yao kuhusu mauaji ya kimbari yanaotekelezwa na Israel huko Gaza. Waandamanaji wanaounga mkono Wapalestina walishiriki katika "Hatua ya Dharura Kwa Ajili ya Rafah" na walielezea hasira zao mbele ubalozi wa utawala ghasibu Israel. Waandamnaji waliokuwa na hasira walivurumisha mabomu ya kujitengenezea ya Molotov Cocktail katika jengo la ubalozi huo wa Israel. Aidha waandamanaji waliwarushia mawe polisi wa kutuliza ghasia ili kulipiza kisasi baada ya kurushiwa  mabomu yakuwarushia vitoa machozi. Mexico, siku ya Jumanne, iliwasilisha tamko la kujiunga na kesi ya Afrika Kusini dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ikiishutumu Israel kwa kutekeleza "mauaji ya kimbari" Gaza. Maandamano kama hayo

Wataalamu zaidi ya 50 wa UN wataka Israel iwekewe vikwazo na marufuku ya silaha

Image
Wataalamu zaidi ya 50 wa Umoja wa Mataifa wametoa mwito wa kuchukuliwa "hatua madhubuti kimataifa" baada ya kuelezea walivyokasirishwa na shambulio la kinyama la jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel ambalo liliua Wapalestina wasiopungua 45 waliokuwa wametafuta hifadhi kwenye kambi ya muda huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Ghaza. Wataalamu hao wa UN wamesema: "picha za kutisha za uharibifu, watu kubaki bila makazi na vifo zimeibuka kutoka Rafah, zikiwemo za watoto wachanga walioraruliwa vipandevipande na watu kuteketezwa wakiwa hai". Kundi hilo la wataalamu zaidi ya 50 wa Umoja wa Mataifa limeendelea kueleza katika taarifa yake kwamba, ripoti zilizotoka kwenye eneo lililolengwa zinaonyesha kuwa shambulio la jeshi la Kizayuni lilikuwa la kiholela na lisilo na mlingano, na lilifanywa wakati watu wakiwa wamekwama ndani wakiungua kwenye mahema ya plastiki, na kusababisha vifo v

Kamati Kuu ya kuchunguza ajali ya helikopta iliyombeba Shahidi Ebrahim Raisi yatoa ripoti ya pili

Image
  May 30, 2024 03:40 UTC Kituo cha Mawasiliano cha Kamandi Kuu ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kimetoa ripoti ya pili ya Kamisheni Kuu ya kuchunguza sababu za ajali ya helikopta iliyosababisha kifo cha Rais Seyed Ebrahim Raisi, na ujumbe ulioandamana naye. Helikopta iliyokuwa imembeba Rais Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje Amir-Abdollahian, Imamu wa Swala ya Ijumaa ya Tabriz Ayatullah Mohammad Ali Al-e-Hashem, Gavana wa Azarbaijan Mashariki Malek Rahmati, kamanda wa kikosi cha walinzi wa rais, marubani wawili na walinzi ilianguka mkoa wa kaskazini-magharibi wa Azarbaijan Mashariki mnamo Mei 19, 2024. Miili yao ilipatikana siku ya Jumatatu baada ya msako wa usiku mzima katika eneo lililokuwa na hali mbaya ya hewa. Wote waliokuwamo ndani ya helikopta hiyo walipoteza maisha na kupata daraja ya juu ya kufa shahidi. Kwa mujibu wa ripoti ya pili iiliyotangazwa Jumatano na Kamati Kuu ya Kuchun

Ndege nyingine isiyo na rubani ya MQ-9 ya Marekani iliyodunguliwa na Yemen wakati wa kampeni ya kuiunga mkono Palestina

Image
    Ndege nyingine isiyo na rubani ya MQ-9 ya Marekani iliyodunguliwa na Yemen wakati wa kampeni ya kuiunga mkono Palestina Yemen imeangusha ndege nyingine ya kisasa isiyo na rubani ya jeshi la Marekani wakati kampeni yake ya kuunga mkono Palestina ikipanuka katikati ya vita vya kikatili vya Israel dhidi ya Gaza. Vikosi vya jeshi la Yemen vilitoa taarifa siku ya Jumatano vikisema kuwa Vikosi vyake vya Ulinzi wa Anga viliidungua ndege isiyo na rubani ya MQ-9 Reaper mapema siku hiyo ilipokuwa ikiruka angani katika jimbo la kati la Marib. "Operesheni ya kulenga shabaha ilifanywa kwa kombora lililotengenezwa nchini kutoka ardhini hadi angani," ilisema taarifa hiyo, na kuongeza kuwa video ya ufyatuaji huo itachapishwa hivi karibuni. Ilikuwa ni mara ya pili kwa siku ambapo Wayemeni waliiangusha MQ-9 Reaper, ndege nzito na ya kisasa yenye thamani ya karibu dola milioni 30. Jumla ya ndege sita zisizo na rubani za aina hii zimesambaratishwa na Yemen tangu mwaka jana wakati nchi hiyo y

Naibu waziri wa fedha wa Marekani amewasili Ukrain

Image
  Adeyemo alisema Marekani inapanga kuchukua hatua zaidi ili kuweka shinikizo kwa uchumi wa Russia. Naibu Waziri wa Fedha wa Marekani Wally Adeyemo amewasili Kyiv siku ya Jumatano kukutana na maafisa wa Ukraine kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha vikwazo dhidi ya Russia pamoja na msaada wa kifedha kwa Ukraine. Alisema Marekani inapanga kuchukua hatua zaidi ili kuweka shinikizo kwa uchumi wa Russia. Uchumi wa Russia umekuwa uchumi wa wakati wa vita, ambapo kila njia ya uzalishaji na viwanda sasa imejikita katika kujenga silaha za kupambana na vita vyao ilivyovichagua na uvamizi hapa Ukraine, Adeyemo alisema Jumatano katika mji mkuu wa Ukraine. “Tunahitaji kufanya kila tuwezalo ili tufanikiwe baada ya hapo”. Adeyemo amesema kipaumbele cha Hazina ni kupunguza mapato ya Russia na kuizuia Russia kupata bidhaa inazozihitaji ili kuzisaidia ngome zake za viwanda vya ulinzi, ikijumuisha bidhaa za matumizi ya nchi mbili kutoka China.

Dhahabu ya Afrika yenye thamani ya mabilioni ya dola husafirishwa kimagendo kila mwaka-ripoti

Image
  Dhahabu ya Afrika yenye thamani ya mabilioni ya dola inauzwa kwa njia ya magendo nje ya bara hilo kila mwaka, nyingi ikipelekwa Dubai kabla ya kusafirishwa kwa njia halali kwenda nchi nyingine, shirika lisilo la serikali kutoka Uswisi limesema Alhamisi. Shirika lisilo la serikali la maendeleo la Uswisi Swissaid lilichapisha ripoti likisema kwamba kati ya tani 321 na 474 za dhahabu kutoka Afrika inayozalishwa kupitia uchimbaji kwa kutumia mikono kwenye migodi midogo inasafirishwa kimagendo kila mwaka, na thamani yake ni kati ya dola bilioni 24 na bilioni 35. Afrika ni mzalishaji mkubwa wa dhahabu duniani, huku Ghana, Afrika Kusini, Mali na Burkina Faso zikiongoza kwa uzalishaji huo mwaka 2022. Kulingana na shirika hilo la Uswisi, usafirishaji wa dhahabu ya Afrika kwa njia ya magendo umeongezeka, uliongezeka maradufu kati ya 2012 na 2022.” Shirika hilo linasema madini hayo ya thamani ni “chanzo cha mapato kwa mamilioni ya wachimbaji wadogo, ni chanzo kikuu cha mapato