Posts

Showing posts from March, 2024

Viongozi wa harakati za Palaestina za Hamas na Jihad Islami wakutana Tehran

Image
  Ismail Haniyah, mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amekutana mjini Tehran na Katibu Mkuu wa Harakati ya Palestina ya Jihad Islami Ziyad al-Nakhaleh.   Hamas ilisema katika taarifa yake siku ya Ijumaa kwamba mkutano huo ulilenga kujadili matukio ya kisiasa na ya medani kuhusiana na vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelezwa na utawala haramu wa Israel dhidi ya watu wa Gaza. Wajumbe wa pande zote mbili wamesifu harakati za muqawama na watu wa Gaza katika kukabiliana na uvamizi wa Israel. Taarifa hiyo imesema: "Aidha, viongozi hao wawili wamejadili juhudi za kukomesha vita, na kusisitiza kwamba mafanikio ya mazungumzo yoyote yasiyo ya moja kwa moja yanategemea mambo manne ya kimsingi: kusimamishwa kabisa vita, kuondoka kikamilifu wanajeshi vamizi wa Isarel katika ukanda wote wa Gaza; kurudi kwa watu waliokimbia makazi yao, kuingia misaada na mahitaji ya msingi kwa watu wa gaza, pamoja na kubadilishana wafung

Hizbullah yajibu mapigo, yashambulia vitongoji vya walowezi wa Kizayuni

Image
    Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imefanya mashambulizi kadhaa dhidi ya vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na kambi kadhaa za Israel kaskazini mwa maeneo yaliyokaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu mwaka 1948, kama sehemu ya awamu nyingine ya operesheni za kulipiza kisasi dhidi ya utawala huo na kuwatetea watu wa Gaza. Taarifa iliyotolewa na Hizbullah imesema kwamba, imelenga vitongoji vya walowezi vya Shlomi na Goren ikijibu mashambulizi yaliyofanywa na Israel dhidi ya raia, hasa mashambulizi ya utawala huo katili katika miji ya Naqoura na Tayr Harfa ambayo yameua takriban wahudumu tisa wa Hizbullah na harakati ya Amal. Wapiganaji wa Hizbullah pia Alhamisi iliyopita walishambulia kituo cha kamandi ya jeshi la Israel kilichoundwa hivi karibuni huko Liman, katika eneo la Magharibi mwa Galilaya, kuwaunga mkono watu wa Gaza. Hizbullah pia imetoa mkanda wa video uliowarekodi wapiganaji wake wakilenga mkusanyiko wa wanajeshi wa Israel huko Horsh Ramim karibu na

Ripoti: Magaidi walioua watu 143 Moscow walipokea maagizo kutoka Ukraine

Image
    Ripoti ya wachunguzi wa Russia imethibitisha kuwepo ushahidi kwamba magaidi walioshambulia ukimbi wa Crocus jijini Moscow walipokea fedha kwa siri kutoka Ukraine, nchi muitifaki wa Marekani ambayo iko vitani na Russia. Hayo yamedokezwa na Kirill Kabanov, mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Kupambana na Rushwa ya Russia ambaye amesema katika mahojiano na Sputnik kwamba data katika vifaa vya kiufundi vilivyonaswa kutoka kwa washukiwa wa shambulio hilo la kigaidi imethibitisha uhusiano wa magaidi hao na Ukraine. Takwimu za awali zilizopokelewa kutoka kwa waliokamatwa katika kesi inayohusiana na shambulio hilo la kigaidi zilionyesha Ukraine ilihusika pakubwa katika shambulio hilo. Kabanov amebainisha kuwa ripoti mpya ya Kamati ya Uchunguzi ya Russia inabainisha kuwa mashirika ya kijasusi ya Ukrine yamehusika katika kuratibu hujuma hiyo ya kigaidi na kuwa ni muhimu kufahamu kuwa mashirika hayo ya kijasusi ya Ukraine yana uhusiano wa moja kwa moja na shirika ku

Wapiganaji wa Muqawama Iraq washambulia kituo 'muhimu' cha kijeshi cha Israel

Image
  Kundi la Wapiganaji wa Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) Iraq limetangaza kushambulia kituo "muhimu" cha kijeshi cha utawala wa Israel kilichoko kaskazini mwa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu katika kuendelea kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, ambao wanastahimili vita vya mauaji ya halaiki ya Israel. Kundi hilo la Iraq ambalo ni mwavuli wa makundi ya kupambana na ugaidi nchini humo limetoa tangazo hilo katika taarifa mapema leo Jumapili. Taarifa hiyo inasema ndege kadhaa zisizo na rubani zimelenga eneo la Eilabun ambapo kituo cha jeshi la Israel hapo kimepata hasara kubwa. Kundi la Wapiganaji wa Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) Iraq lilihitimisha taarifa hiyo kwa kusema kwamba operesheni hiyo imefanywa "kwa mshikamano na watu wa Gaza." Kundi hilo limekuwa likifanya mashambulizi mengi ya aina hiyo tangu tarehe 7 Oktoba, wakati utawala haramu wa Isarel ulipoanzisha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa

Jihad Islami: Wapalestina hawangeweza kusimama dhidi ya Israel bila ya kuungwa mkono na Iran

Image
    Kiongozi mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina ametangaa bayana kuwa watu wa Palestina hawangeweza kusimama dhidi ya utawala haramu wa Israel kama kusingekuwa na uungaji mkono kamili wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Islami  ya Palestina Ziyad al-Nakhaleh aliyasema hayo jana Jumamosi katika mkutano na waandishi wa habari akiwa na Hossein Amir-Abdollahian Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran mjini Tehran. Amepongeza nafasi muhimu ya Iran katika kuunga mkono muqawama au mapambano ya wananchi wa Palestina tangu utawala wa Israel ulipoanzisha vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya watu wa Gaza mapema Oktoba 2023. Amebaini kuwa diplomasia hai ya Iran imechukua nafasi kubwa katika kufafanua msimamo wa harakati za kupigania ukombozi wa Palestina. Kiongozi huyo wa Jihad Islami amesisitiza kuwa wananchi wa Palestina watapata ushindi wa mwisho katika vita vyao dhidi ya Israel na kusema kuwa kusimama kidete Wapalestina kutakuwa kigezo

FAB-3000: Urusi imeanza kutumia tena mabomu hatari

Image
      Moja ya sababu za kuanguka mikononi mwa Urusi mji wa Avdeevka ni mashambulio makubwa ya angani. Makombora ya FAB-500 yana uzito wa nusu tani. Wanaharibu majengo na barabara. Vifaa vya Kikosi cha Wanajeshi wa Ukraine, vilivyoko kilomita moja kabla ya mstari wa mbele viliharibiwa vibaya. Jeshi la Anga la Kikosi cha Wanajeshi wa Ukraine katika miezi ya hivi karibuni lilitangaza kuangusha ndege 13 za kivita za Urusi. Hivi karibuni, chaneli ya Urusi ya Wizara ya Ulinzi, iliripoti kwamba Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu alitembelea moja ya kiwanda kikubwa cha kijeshi.   Ripoti hiyo ilizungumza juu ya kuongezeka mara mbili utengenezaji wa makombora ya FAB-1500, lakini zaidi ya yote ilieleza juu ya habari kuhusu kuanza tena kwa mradi wa FAB-3000. Mabomu haya kutoka angani yana kilo 1,400 za vilipuzi - yana uwezo mkubwa wa kufanya uharibifu.   Jeshi la Soviet lilitumia mabomu kama hayo wakati wa uvamizi wa Afghanistan katika miaka ya 1980. Kwa makombora hayo, waliizingira Kabu

Vikosi maalum vya majeshi ya Urusi,Iran na China vilivyookoa meli iliyo...

Image

Urusi imeipa Yemen kombora la Hypersonic?yemen kutumia kombora la Hypers...

Image