Posts

Uchaguzi mpya unaweza kuchukua hadi miaka minne, kiongozi wa waasi wa Syria anasema

Image
  Chanzo cha picha, Reuters Maelezo ya picha, Alisema hajioni kuwa "mkombozi wa Syria", akiongeza kuwa watu wamejiokoa Uchaguzi mpya nchini Syria unaweza kuchukua hadi miaka minne, kiongozi wa waasi Ahmed al-Sharaa amesema katika mahojiano ya matangazo. Hii ni mara yake ya kwanza kutoa ratiba ya uchaguzi unaowezekana nchini Syria tangu kundi lake la Hayat Tahrir al-Sham (HTS) liongoze mashambulizi ya waasi yaliyomuondoa madarakani aliyekuwa Rais Bashar al-Assad. Katika mahojiano na shirika la utangazaji la serikali ya Saudi Al Arabiya siku ya Jumapili, alisema kuandaa katiba mpya kunaweza kuchukua hadi miaka mitatu. Alisema pia inaweza kuchukua mwaka mmoja kabla ya Wasyria kuanza kuona mabadiliko makubwa na maboresho ya huduma za umma kufuatia kupinduliwa kwa utawala wa Assad. Sharaa alisema Syria inahitaji kujenga upya mfumo wake wa sheria na italazimika kufanya sensa kamili ya watu ili kuendesha uchaguzi halali.

Hawa ndio wanaume 10 matajiri zaidi barani Afrika

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Mabilionea wa Kiafrika, hupata utajiri kwa kutumia fursa za biashara zinazopatikana kwao katika bara ambalo limekuwa mgodi wa dhahabu na kwingineko duniani. Saa 1 iliyopita Isidore Kouwonou BBC Afrique Wamefanya kazi kwa bidii ili kuwa mahali walipo leo. Wanaume hawa ni matajiri zaidi duniani na barani Afrika. Wanaume hawa wameweza kukaa katika mkondo huo licha ya ugumu unaohusishwa na mvutano wa kimataifa, kuongezeka kwa mfumuko wa bei miongoni mwa nchi za bara, kushuka kwa sarafu za ndani dhidi ya sarafu kuu, hali ngumu kwenye masoko ya kifedha, nk. Matangazo Mabilionea wa Afrika, kwa kuwa ndio tunaowazungumzia, wameweza kufikia utajiri huu kwa kutumia fursa za biashara zinazopatikana katika bara hili ambalo limekuwa mgodi wa dhahabu na kwingineko duniani. Tunakuletea kwako orodha ya 2024 iliyoanzishwa na ya kipimo cha Bloomberg cha mabilionea Billionaires Index cha matajiri wakubwa ambao utajiri wao ni unafi...

Tetesi za soka Jumatatu: Alexander-Arnold akaribia kusaini mkataba na Real Madrid

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Saa 1 iliyopita Beki wa kulia wa Liverpool Trent Alexander-Arnold, 26, yuko mbioni kusaini mkataba na Real Madrid , huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza akiendelea kupuuza ofa mpya za kuongeza mkataba wake wa sasa unaomalizika msimu huu wa joto. (AS - in Spanish) Liverpool itawanunua beki wa Bayer Leverkusen Mholanzi Jeremie Frimpong na beki wa Bayern Munich Alphonso Davies, wote 24, ikiwa Alexander-Arnold atajiunga na kikosi hicho cha Madrid. (Team talk) Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Nigeria Ola Aina Manchester City wanammfuatilia beki wa kulia wa kimataifa wa Nottingham Forest wa Nigeria Ola Aina, 28, kama kiungo mbadala wa Muingereza Kyle Walker, 34. (Sun) Mshambuliaji wa Ureno na Al-Nassr Cristiano Ronaldo, 39, amekataa kukataa kuhamia Manchester City , licha ya kuwa amewachezea wapinzani wake Manchester United kwa misimu miwili. (Talksport) Newcastle United wanavutiwa na beki wa kati wa Lens Abdukod...

Ahadi ya Al-Joulani ya kushirikisha Wasyria wote katika uendeshaji nchi imethibiti kuwa ni uongo

Image
  Kwa kuanza kwa wimbi la timuatimua ya maafisa wa jamii ya Maalawi katika wizara za serikali ya Syria, imethibiti kuwa ahadi alizokuwa ametoa Abu Muhammad Al-Jolani za kutotengwa tabaka lolote la jamii ya Wasyria katika uendeshaji nchi ni za uongo. Al-Jolani, ambaye ni kiongozi wa kundi la kigaidi la Tahrir al-Sham, alikuwa hapo awali amedai kwamba, hana nia ya kulitenga kundi au tabaka lolote la Wasyria, lakini viongozi wa jamii ya Maalawi wamewekwa kando katika orodha mpya iliyotolewa ya majina ya maafisa 34 wa nchi hiyo ambayo imeandaliwa kwa kutumia vigezo na utashi wa kidini na kimadhehebu.   Duru za ndani ya Syria zimetangaza kuwa al-Jolani na wahusika walio chini ya uongozi wake wanatekeleza sera ya kuhakikisha hakuna afisa yeyote wa jamii ya Maalawi anayesalia katika taasisi ya serikali.   Kwa mujibu wa duru hizo, sera hiyo ya al-Jolani in...

Intelijensia ya Russia: US na UK zinapanga mashambulio ya kigaidi dhidi ya vituo vyetu vilivyoko Syria

Image
  Idara ya Intelijensia ya Russia ya Nje ya Nchi (SVR) imetahadharisha kuwa Marekani na Uingereza zinapanga mashambulizi ya kigaidi katika vituo ya kijeshi vya nchi hiyo vilivyoko Syria ili hali ya nchi hiyo isitangamae na amani na uthabiti usirejee nchini humo. Katika taarifa iliyotoa siku ya Jumamosi, SVR imesema, tangu ilipoanguka serikali ya Rais Bashar Assad wa Syria mapema mwezi huu, Washington na London zimeweka lengo la "kudumisha machafuko katika Mashariki ya Kati" ili kulihodhi na kulidhibiti kwa sura ya kudumu eneo hilo.   Hata hivyo, -kwa mujibu wa taarifa hiyo- uwepo wa kijeshi wa Russia kwenye pwani ya Mediterania ya Syria umekuwa ukikwamisha mipango yao.   Idara ya Intelijensia ya Russia ya Nje ya Nchi imeendelea kufichua kuwa, ili kuondoa kikwazo hicho, Idara za Ujasusi za Uingereza zinaratibu mipango ya kuandaa mfululizo wa mashambulizi ya...

Makubaliano ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China ya kutekeleza mpango wa kistratejia wa nchi mbili

Image
  Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China wametathimini kuwa chanya mchakato unaopiga hatua wa kutekeleza vipengee vya ushirikiano wa kistratejia katika miaka ya karibuni. Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye yuko ziarani nchini China akiongoza ujumbe rasmi wa ngazi amekutana na kufanya mazungumzo na Wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo. Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran China wamesisitiza katika mazungumzo hayo kuwa watafanya juhudi kutekeleza mpango wa ushirikiano wa kina kati ya nchi mbili katika kivuli cha miongozo ya kimkakati ya viongozi wa nchi  mbili na  kuimarisha mabadilishano ya tajiriba za kiuongozi na kiutendaji katika nyanja za kisiasa, kidiplomasia, kibunge, kiulinzi, kiusalama, kijeshi, masuala ya anga, uchumi na biashara. Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya I...

Jeshi la IRGC lasema liko tayari kulinda usalama wa Iran

Image
  Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeeleza utayari wake kamili wa kulinda usalama wa Iran na kukabiliana na njama za adui anayelenga kuleta machafuko na uchochezi nchini. Katika taarifa iliyotolewa Jumapili, IRGC iliangazia kumbukumbu ya maandamano ya kitaifa ya kuunga mkono serikali yaliyofanyika mwaka a 2009 katika tarehe tisa ya mwezi wa Dey wa kalenda ya Kiajemi, ambayo ni sawa na Desemba 30. IRGC imetaja Hamasa ya Dey 9 kama tukio la "utukufu na kuamua hatma" ambalo lilishangaza "mtandao wa uovu na jinai wa wahaini wanaopata himaya ya Marekani na Wazayuni". Mnamo Desemba 30, 2009, mamilioni ya Wairani walikusanyika katika mji mkuu Tehran na miji mingine kumaliza miezi kadhaa ya ghasia za baada ya uchaguzi na kuonyesha utiifu wao kwa serikali ya Kiislamu. Machafuko yaliyoungwa mkono na nchi za kigeni yalipangwa na Mehdi Karroubi na Mir ...