Posts

Showing posts from December, 2024

Uchaguzi mpya unaweza kuchukua hadi miaka minne, kiongozi wa waasi wa Syria anasema

Image
  Chanzo cha picha, Reuters Maelezo ya picha, Alisema hajioni kuwa "mkombozi wa Syria", akiongeza kuwa watu wamejiokoa Uchaguzi mpya nchini Syria unaweza kuchukua hadi miaka minne, kiongozi wa waasi Ahmed al-Sharaa amesema katika mahojiano ya matangazo. Hii ni mara yake ya kwanza kutoa ratiba ya uchaguzi unaowezekana nchini Syria tangu kundi lake la Hayat Tahrir al-Sham (HTS) liongoze mashambulizi ya waasi yaliyomuondoa madarakani aliyekuwa Rais Bashar al-Assad. Katika mahojiano na shirika la utangazaji la serikali ya Saudi Al Arabiya siku ya Jumapili, alisema kuandaa katiba mpya kunaweza kuchukua hadi miaka mitatu. Alisema pia inaweza kuchukua mwaka mmoja kabla ya Wasyria kuanza kuona mabadiliko makubwa na maboresho ya huduma za umma kufuatia kupinduliwa kwa utawala wa Assad. Sharaa alisema Syria inahitaji kujenga upya mfumo wake wa sheria na italazimika kufanya sensa kamili ya watu ili kuendesha uchaguzi halali.

Hawa ndio wanaume 10 matajiri zaidi barani Afrika

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Mabilionea wa Kiafrika, hupata utajiri kwa kutumia fursa za biashara zinazopatikana kwao katika bara ambalo limekuwa mgodi wa dhahabu na kwingineko duniani. Saa 1 iliyopita Isidore Kouwonou BBC Afrique Wamefanya kazi kwa bidii ili kuwa mahali walipo leo. Wanaume hawa ni matajiri zaidi duniani na barani Afrika. Wanaume hawa wameweza kukaa katika mkondo huo licha ya ugumu unaohusishwa na mvutano wa kimataifa, kuongezeka kwa mfumuko wa bei miongoni mwa nchi za bara, kushuka kwa sarafu za ndani dhidi ya sarafu kuu, hali ngumu kwenye masoko ya kifedha, nk. Matangazo Mabilionea wa Afrika, kwa kuwa ndio tunaowazungumzia, wameweza kufikia utajiri huu kwa kutumia fursa za biashara zinazopatikana katika bara hili ambalo limekuwa mgodi wa dhahabu na kwingineko duniani. Tunakuletea kwako orodha ya 2024 iliyoanzishwa na ya kipimo cha Bloomberg cha mabilionea Billionaires Index cha matajiri wakubwa ambao utajiri wao ni unafi...

Tetesi za soka Jumatatu: Alexander-Arnold akaribia kusaini mkataba na Real Madrid

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Saa 1 iliyopita Beki wa kulia wa Liverpool Trent Alexander-Arnold, 26, yuko mbioni kusaini mkataba na Real Madrid , huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza akiendelea kupuuza ofa mpya za kuongeza mkataba wake wa sasa unaomalizika msimu huu wa joto. (AS - in Spanish) Liverpool itawanunua beki wa Bayer Leverkusen Mholanzi Jeremie Frimpong na beki wa Bayern Munich Alphonso Davies, wote 24, ikiwa Alexander-Arnold atajiunga na kikosi hicho cha Madrid. (Team talk) Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Nigeria Ola Aina Manchester City wanammfuatilia beki wa kulia wa kimataifa wa Nottingham Forest wa Nigeria Ola Aina, 28, kama kiungo mbadala wa Muingereza Kyle Walker, 34. (Sun) Mshambuliaji wa Ureno na Al-Nassr Cristiano Ronaldo, 39, amekataa kukataa kuhamia Manchester City , licha ya kuwa amewachezea wapinzani wake Manchester United kwa misimu miwili. (Talksport) Newcastle United wanavutiwa na beki wa kati wa Lens Abdukod...

Ahadi ya Al-Joulani ya kushirikisha Wasyria wote katika uendeshaji nchi imethibiti kuwa ni uongo

Image
  Kwa kuanza kwa wimbi la timuatimua ya maafisa wa jamii ya Maalawi katika wizara za serikali ya Syria, imethibiti kuwa ahadi alizokuwa ametoa Abu Muhammad Al-Jolani za kutotengwa tabaka lolote la jamii ya Wasyria katika uendeshaji nchi ni za uongo. Al-Jolani, ambaye ni kiongozi wa kundi la kigaidi la Tahrir al-Sham, alikuwa hapo awali amedai kwamba, hana nia ya kulitenga kundi au tabaka lolote la Wasyria, lakini viongozi wa jamii ya Maalawi wamewekwa kando katika orodha mpya iliyotolewa ya majina ya maafisa 34 wa nchi hiyo ambayo imeandaliwa kwa kutumia vigezo na utashi wa kidini na kimadhehebu.   Duru za ndani ya Syria zimetangaza kuwa al-Jolani na wahusika walio chini ya uongozi wake wanatekeleza sera ya kuhakikisha hakuna afisa yeyote wa jamii ya Maalawi anayesalia katika taasisi ya serikali.   Kwa mujibu wa duru hizo, sera hiyo ya al-Jolani in...

Intelijensia ya Russia: US na UK zinapanga mashambulio ya kigaidi dhidi ya vituo vyetu vilivyoko Syria

Image
  Idara ya Intelijensia ya Russia ya Nje ya Nchi (SVR) imetahadharisha kuwa Marekani na Uingereza zinapanga mashambulizi ya kigaidi katika vituo ya kijeshi vya nchi hiyo vilivyoko Syria ili hali ya nchi hiyo isitangamae na amani na uthabiti usirejee nchini humo. Katika taarifa iliyotoa siku ya Jumamosi, SVR imesema, tangu ilipoanguka serikali ya Rais Bashar Assad wa Syria mapema mwezi huu, Washington na London zimeweka lengo la "kudumisha machafuko katika Mashariki ya Kati" ili kulihodhi na kulidhibiti kwa sura ya kudumu eneo hilo.   Hata hivyo, -kwa mujibu wa taarifa hiyo- uwepo wa kijeshi wa Russia kwenye pwani ya Mediterania ya Syria umekuwa ukikwamisha mipango yao.   Idara ya Intelijensia ya Russia ya Nje ya Nchi imeendelea kufichua kuwa, ili kuondoa kikwazo hicho, Idara za Ujasusi za Uingereza zinaratibu mipango ya kuandaa mfululizo wa mashambulizi ya...

Makubaliano ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China ya kutekeleza mpango wa kistratejia wa nchi mbili

Image
  Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China wametathimini kuwa chanya mchakato unaopiga hatua wa kutekeleza vipengee vya ushirikiano wa kistratejia katika miaka ya karibuni. Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye yuko ziarani nchini China akiongoza ujumbe rasmi wa ngazi amekutana na kufanya mazungumzo na Wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo. Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran China wamesisitiza katika mazungumzo hayo kuwa watafanya juhudi kutekeleza mpango wa ushirikiano wa kina kati ya nchi mbili katika kivuli cha miongozo ya kimkakati ya viongozi wa nchi  mbili na  kuimarisha mabadilishano ya tajiriba za kiuongozi na kiutendaji katika nyanja za kisiasa, kidiplomasia, kibunge, kiulinzi, kiusalama, kijeshi, masuala ya anga, uchumi na biashara. Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya I...

Jeshi la IRGC lasema liko tayari kulinda usalama wa Iran

Image
  Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeeleza utayari wake kamili wa kulinda usalama wa Iran na kukabiliana na njama za adui anayelenga kuleta machafuko na uchochezi nchini. Katika taarifa iliyotolewa Jumapili, IRGC iliangazia kumbukumbu ya maandamano ya kitaifa ya kuunga mkono serikali yaliyofanyika mwaka a 2009 katika tarehe tisa ya mwezi wa Dey wa kalenda ya Kiajemi, ambayo ni sawa na Desemba 30. IRGC imetaja Hamasa ya Dey 9 kama tukio la "utukufu na kuamua hatma" ambalo lilishangaza "mtandao wa uovu na jinai wa wahaini wanaopata himaya ya Marekani na Wazayuni". Mnamo Desemba 30, 2009, mamilioni ya Wairani walikusanyika katika mji mkuu Tehran na miji mingine kumaliza miezi kadhaa ya ghasia za baada ya uchaguzi na kuonyesha utiifu wao kwa serikali ya Kiislamu. Machafuko yaliyoungwa mkono na nchi za kigeni yalipangwa na Mehdi Karroubi na Mir ...

Takriban watu 120 wafariki katika ajali ya ndege Korea Kusini

Image
  Chanzo cha picha, Reuters/Yonhap Ndege iliyokuwa imebeba abiria 181 imeanguka katika uwanja wa ndege kusini magharibi mwa Korea Kusini. Ajali hiyo ilitokea muda mfupi baada ya 09:00 saa za eneo - 00:00 GMT - wakati ilipokuwa ikitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Muan. Picha zinaonekana kuonyesha ndege hiyo ikiteleza kutoka kwenye njia ya kurukia na kuangukia ukuta, kabla ya baadhi ya sehemu zake kuwaka moto. Shirika la Kitaifa la Zimamoto limethibitisha sasa kwamba watu 167 walifariki katika ajali hiyo ya ndege. Hapo awali, tulisikia pia kwamba wafanyikazi wawili wa ndege walipatikana wakiwa hai na kusafirishwa hadi hospitalini. Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Muan wa ukubwa wa kati ulifunguliwa mwaka wa 2007, na una njia za kwenda nchi kadhaa za A

Hii inaweza kuwa ajali mbaya zaidi ya ndege nchini Korea Kusini

  Jean Mackenzie Mwanahabari wa Seoul Ajali hii si ya kawaida kwa Korea Kusini, ambayo imekuwa na rekodi nzuri ya usalama wa ndege katika miaka ya hivi karibuni. Ikiwa idadi ya vifo itathibitishwa, hii itakuwa ajali mbaya zaidi ya ndege kuwahi kutokea katika ardhi ya Korea Kusini. Inaonekana pia kuwa ajali mbaya pekee ambayo Jeju Air imepata katika historia yake ya karibu miaka 20. Jeju Air ndilo shirika maarufu la ndege la bei nafuu nchini Korea Kusini, lenye safari nyingi za ndege katika eneo lote la Asia. Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo alisema katika mkutano na wanahabari hapo awali shirika hilo la ndege halikuwa na historia ya ajali. Aliomba msamaha kwa familia za waathiriwa.

Shirika la ndege la Jeju Air laomba msamaha kwa ajali

Image
  Chanzo cha picha, EPA/Yonhap Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ndege la Jeju Air ameomba msamaha hadharani kwa waathiriwa wa ajali hiyo. Katika mkutano mfupi wa wanahabari, Kim E-bae na wakuu wengine wa kampuni waliinamisha vichwa vyao na kusema kuwaunga mkono wafiwa ndio kipaumbele chao kwa sasa. "Sisi Jeju Air tunainamisha vichwa vyetu kwa kuomba msamaha kwa kila mtu ambaye ameathirika katika tukio hili kwenye Uwanja wa Ndege wa Muan," inasema taarifa hiyo ambayo imetafsiriwa kwa Kiingereza. "Tutafanya kila tuwezalo kujibu tukio hilo. Tunasikitika kwa mfadhaika." Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana, lakini vyombo vya habari nchini humo viliripoti kuwa huenda ilisababishwa na ndege kukamatwa kwenye mfumo wa ndege hiyo. Ajali hii ya kwanza mbaya katika historia ya Jeju Air, mojawapo ya mashirika makubwa ya ndege ya bei ya chini ya Korea Kusini, ambayo ilianzishwa mwaka 2005

Kaimu rais awasili eneo la ajali

Image
  Chanzo cha picha, EPA/Yonhap Kaimu Rais wa Korea Kusini Choi Sang-mok amefika katika eneo la ajali, ofisi ya rais inasema. Choi alitoa mwelekeo wa kutoa wafanyikazi, huduma ya afya na vifaa vya kusaidia katika juhudi za uokoaji, ofisi inasema. Serikali itafanya yote iwezayo kusaidia familia zilizofiwa, inaongeza. Choi aliteuliwa kuwa kiongozi wa muda wa nchi hiyo siku ya Ijumaa baada ya aliyekuwa kaimu rais kuondolewa madarakani kutokana na mzozo wa kisiasa unaoendelea.

Katika picha: Familia zinaomboleza huku wafanyakazi wakitafuta mabaki

Image
  Katika picha: Familia zinaomboleza huku wafanyakazi wakitafuta mabaki Siku nzima tumekuwa tukipokea picha mpya kutoka eneo la ajali huko Muan, Korea Kusini. Jamaa za waliofariki kwenye ajali hiyo wamekusanyika kwenye uwanja wa ndege. Chanzo cha picha, Reuters Chanzo cha picha, Reuters Chanzo cha picha, Reuters Chanzo cha picha, Reuters

Rais anayeondoka wa Georgia akataa kujiuzulu huku mrithi wake akiapishwa

Image
  Chanzo cha picha, Reuters/EPA Maelezo ya picha, Mikheil Kavelashvili (kushoto) aliapishwa kama rais wa Georgia, Salome Zourabichvili (kulia) Rais anayemaliza muda wake Maelfu ya wananchi wa Georgia wameandamana katika mji mkuu wa Tbilisi huku rais mpya wa chama tawala cha Georgian Dream party akiapishwa. Mikheil Kavelashvili, mchezaji soka wa zamani, ameapishwa katika kipindi kigumu cha kisiasa nchini humo baada ya serikali kusitisha ombi lake la kujiunga na Umoja wa Ulaya. Georgian Dream kilishinda uchaguzi wa bunge mwezi Oktoba, lakini ushindi huo uligubikwa na madai ya udanganyifu ambayo tangu wakati huo yamesababisha maandamano mitaani. Rais anayemaliza muda wake Salome Zourabichvili alikataa kujiuzulu siku ya Jumapili, akisema ndiye "rais pekee halali". Akihutubia umati uliokusanyika nje, Zourabichvili alisema ataondoka ikulu ya rais lakini akamtaja mrithi wake kuwa haramu.

Je kuna faida ya kula manjano na viungo vingine?

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Utafiti umegundua wanaotumia pilipili karibu kila siku walikuwa na hatari ndogo ya kifo 29 Disemba 2024, 12:54 EAT Imeboreshwa Saa 3 zilizopita Pilipili, manjano na viungo vingine zinadaiwa kuwa na umuhimu katika afya na pia kuboresha “kingamaradhi .” Je viungo vinaongeza virutubisho kwa vyakula au kutukinga na maradhi? Viungo kama manjano, pilipili, na tangawizi vimekuwa sehemu muhimu ya lishe yetu kwa maelfu ya miaka. Hivi karibuni, viungo hivi vimekuwa vikitangazwa kama vyakula vyenye faida za kiafya, na wengi wanadai kwamba vinaweza kuimarisha mfumo wa kinga na kutibu magonjwa. Inasemekana Hillary Clinton alikuwa akipenda kula pilipili moja kwa siku akiwa katika msururu wa kampeini 2016 kama njia moja ya kujikinga na maradhi. Manjano, imekuwa ikitumiwa Asia kwa miongo, na imeanza kutumiwa katika kupika kahawa almaarufu golden lattes.- na wakati wa uviko 19, iliaminika manjano yanaimarisha mfumo wa kinga mwilini na k...

Mji ambao kubeba silaha ni wajibu

Image
  Maelezo ya picha, James Raban ni mmiliki wa duka la bunduki linalomilikiwa na familia ambalo huuza kila kitu kuanzia bastola za Glock hadi gobori ya kale Maelezo kuhusu taarifa Author, Brandon Drenon Nafasi, BBC, Kennesaw, Georgia Saa 4 zilizopita Kennesaw, Georgia, ni mji mdogo wa Kusini Marekani ambao una mambo yote unayoweza kufikiria kuhusu miji ya kanda hii. Harufu ya mikate inayookwa inanukia kutoka kwa tanuri mikate ya Honeysuckle Biscuits & Bakery, sauti ya treni inasikika kwa mbali, na wanandoa wapya wanaacha kadi walizoandika katika mkahawa wakishukuru kwa mazingira ya joto. Lakini kuna jambo moja kuhusu Kennesaw ambalo linaweza kushangaza: sheria iliyopitishwa katika miaka ya 1980 inayowalazimisha wakazi wa mji huu kubeba silaha na bunduki. "Sio kama utakavyobeba silaha kwenye eneo lako," anasema Derek Easterling, meya wa mji huu ambaye anahudumu muhula wake wa tatu na mwenye kusema kwamba yeye ni "mstaafu kutoka Jeshi la Wanamaji." ...

Lulu Hunt Peters, mtaalam wa lishe bora aliyevumbua kuhesabu kalori zaidi ya karne moja iliyopita

Image
  Chanzo cha picha, Getty Images Maelezo ya picha, Lulu Hunt Peters, alihitimu kutoka chuo kikuu cha California wakati wanawake walikuwa chini ya asilimia 5 ya wanafunzi wa udaktari nchini Marekani Maelezo kuhusu taarifa Author, Laura Plitt Nafasi, BBC World 29 Disemba 2024, 09:22 EAT Imeboreshwa Saa 6 zilizopita Idadi ya kalori huonekana kwenye lebo nyingi za vyakula na vinywaji vilivyopakuliwa, na hata kwenye menyu za baadhi ya mikahawa na baa:taarifa za kalori zipo kila mahali. Unaweza kujua ni hatua ngapi unatembea na kuchoma kalori kila siku kwa kutazama kipimo kilichoko kwenye simu yako, na kama unakwenda ukumbi wa michezo ya mazoezi ya viungo, utaona idadi ya kalori zikionekana kwenye kielezo cha baiskeli au kinu cha kuendesha kwa miguu (treadmill) za mazoezi. Lakini hata bila msaada huu, pengine unajua kwamba saladi ya lettuce na nyanya ina kalori kuliko mkate wa nyama na kwamba kukimbia kutachoma kalori zaidi kuliko kutembea. Hata hivyo, kuhesabu kalori iliku...